Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amekagua vivuko viwili kati ya sita (6) vilivyowasili katika eneo la Magogoni kwa ajili ya kutoa huduma ya usafiri eneo la Kigamboni na Magogoni na kuagiza kukamilisha taratibu zote za uendeshaji wa vivuko kwa mujibu wa sheria na kanuni za uendeshaji vyombo vya majini nchini.

Ulega amefanya ukaguzi huo leo tarehe 21 Januari 2025, Jijini Dar es Salaam kabla ya vivuko hivyo kuanza kutumika ambapo pamoja na mambo mengine ameshukuru kampuni ya Azam Marine kwa kuingia ubia na Serikali kupitia vivuko hivyo kwani kutapunguza adha ya usafiri katika eneo hilo.
